Mkristo
lazima atoe zaka? HIli ni swali ambalo limewasumbua wengi, ni swali
ambalo wakati mwingine majibu yake huambatana na vitisho, na shuku
kwamba muulizaji anaroho ya kutokutii maandiko. Walio wengi ujua kuwa
ni lazima mkristo atoe zaka na kutoitoa husababisha laana maishani. Kutokana na kuogopa laana wengi wao hutoa si kwa kupenda na kwa furaha
bali kwa maumivu yasiyokifani, na mara nyingi hutoa kwa kusitasita na
kuruka ruka, hata kuwafanya wapokeaji kutunga sheria au taratibu
zitakazo wabana watoaji waweze kulitoa kwa shuruti hata kama hawapendi.
Wengine wamekwenda mbali zaidi kuwanyima washirika wengine msaada wawapo
katika vipindi vigumu kama kufiwa au kuugua kwa sababu tu hawatoi zaka au kama
wanatoa hawatoi sawa sawa kulingana na rekodi zao.
Somo
hili linalenga kujibu swali hili kwa undani, likianza kwa kutoa
historia ya utoaji wa zaka katika Agano la Kale mpaka wakati wa Agano
Jipya. Katika somo hili utajifunza kuwa mkristo hafungwi na sheria ya
zaka na kwamba utoaji wa mkristo husukumwa na moyo wa furaha na ihari na
kwa kadri Mungu alivyo mbariki. Kwamba mkristo kwa kusukumwa na moyo
huo aweza hata kutoa zaidi ya fungu la kumi maadamu utoaji wake
haukuambatana na shuruti ya namna yoyote!